SlideShare ist ein Scribd-Unternehmen logo
1 von 6
Risala ya Uzinduzi wa Wiki ya Maji Wilayani Bunda

iliyosomwa na Eng. Tanu Deule, Mhandisi wa maji wa wilaya

       ya Bunda kwenye Tengi la Maji la Mlima Kaswaka

                                   Bunda Mjini

                            Tarehe 17 - Machi - 2011

Mh. Mgeni Rasmi (Mkuu wa Wilaya ya Bunda)

Wah. Viongozi mliofika hapa (Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Bunda)

Wafanyakazi wa Mamlaka ya Maji Bunda

Wafanyakazi wenzangu wa Idara ya Maji kwa ujumla wenu

Wafanyakazi wa Halmashauri yetu mliofika hapa kuungana nasi

Ndugu zetu waandishi wa habari

Ndugu Wananchi

Mabibi na mabwana



Tumsifu Yesu Kristo

Asalaam Aleykum

Bwana asifiwe



Kabla ya yote napenda kumshukuru mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa

kutujalia uzima na leo tupo hapa


Mh. Mgeni Rasmi

Leo Halmashauri yetu inaungana na taifa zima kuadhimisha wiki ya maji ambayo

imezinduliwa rasmi na Waziri wa Maji Mh. Prof Mark Mwandosya (MB) kwenye

viwanja vya Nyamagana jijini Mwanza jana tarehe 16/3/2011. Wiki hii ya maji

itahitimishwa tarehe 22/3/2011 ambayo ni siku ya Maji kidunia yaani World Water Day.
Maadhimisho haya ya wiki ya maji ni ya 23 tangu yaanze kufanyika kitaifa mwaka 1988

na kauli mbiu ya mwaka huu ni “Maji kwaajili ya Miji: kukabiliana na changamoto

mbalimbali Mijini”



Mh. Mgeni Rasmi

Miji inayotajwa kwenye kauli mbiu ya mwaka huu ni pamoja na mji wa Bunda. Na hii

ndiyo maana Halmashauri yetu ya Wilaya Ikaonelea kuwa ni vema uzinduzi huu wa

wiki ya maji kiwilaya ufanyike ndani ya viunga hivi vya Mjini na hasa kwenye mradi

mpya wa maji Bunda Mjini.


Mh. Mgeni Rasmi

Kuhusu chombo chenye mamlaka ya kutoa huduma ya maji Bunda mjini

Jukumu la utoaji huduma ya maji hapa Mjini, limekasimiwa kwa Mamlaka ya maji

Bunda mjini yaani Bunda Water Supply Authority. Hii ni Mamlaka kamili

iliyoanzishwa tarehe 21/6/2002 baada ya kutangazwa kwenye gazeti la serikali. Bodi

yake ya kwanza ilianza kutenda kazi tarehe 1Juni 2003 na hivi sasa kuna Bodi ya 3

iliyoteuliwa rasmi tarehe 10 januari mwaka huu wa 2011.


Mh. Mgeni Rasmi

Kuhusu huduma ya maji hapa mjini.

•   Kiwango cha maji yanayozalishwa kwa siku yameongezeka kutoka lita 720,000

    mwaka 2006 hadi liata 1,260,000 mwaka 2010

•   Wateja wameongezeka kutoka 650 mwaka 2006 hadi wateja1,227 mwaka 2010

•   Wastani wa watu wenye maji ya bomba wameongezeka kutoka asilimia 15.4 mwaka

    2006 hadi asilimia 27.4 mwaka 2010



Mh. Mgeni Rasmi

Kuhusu mradi Mpya wa Maji Bunda Mjini


                                         2
Takwimu iliyoonyeshwa hapo juu kwamba katika watu 100 ni watu 27 tu ndo

wanapata maji ya bomba inadhihirisha ukubwa wa tatizo lililopo na kwamba

changamoto hii ni kubwa sana kwetu. Hivyo basi, Halmashauri kwa kushirikiana na

Wizara ya Maji na kwa Msukumo wa pekee wa mheshimiwa Mbunge wa jimbo la

Bunda, Mh. Stephen M. Wasira (MB) na Waziri wa nchi ofisi ya raisi –Mawasiliano na

Uratibu, tumeanza kutekeleza mradi mpya wa maji hapa Bunda mjini utakaokuwa na

chanzo chake kwenye kijiji cha Nyabehu kilichopo umbali wa kilomita 26 kutoka hapa

mjini.



Mradi huu ni mkubwa sana ukiangalia gharama zake hadi hapo utakapo kamilika, na

utaona kuwa umekuwa ukitengewa fedha kidogo hadi kupelekea utekelezwe kwa

awamu kadiri fedha zilivyokuwa zinapatikana, kwani kusubiri fedha hadi zitimie zote

ndiyo mradi uanze kujengwa haukuonekana kuwa ni uamuzi mzuri.



Kwa fedha zilizokuwa zinapatikana, mradi huu umetekelezwa kama ifuatavyo;


Awamu ya I: Zimenunuliwa pampu mpya 9 za kusukuma maji na tayari zipo hapa

            Wilayani Bunda zimetunzwa kwenye Bohari yetu

Awamu ya II: Umefanyika ujenzi wa

           i. Tengi la maji Migungani lenye ujazo wa lita 225,000

           ii. Tengi la kwenye Mlima Kaswaka lenye ujazo wa lita 675,000

          iii. Nyumba ya kufunga pampu (Pump House)

          iv. Nyumba ya wahudumu wa pamp (pump attendant house) na choo yake

           v. Barabara ya kwenda kwenye tengi la maji kwenye Mlima Kaswaka

Awamu ya II: Awamu hii bado haijatekelezwa lakini itahusisha kazi zifuatazo

            •   Ujenzi wa chujio (treatment plant)

            •   Kununua na kulaza mabomba ya bomba kuu kilometa 26

            •   Kusimika pampu

                                          3
•   Kuingiza umeme wenye msongo mkubwa, na

             •   Kusuka mtandao mpya wa usambazaji maji hapa mjini

Mh. Mgeni Rasmi

Awamu hii ya tatu ndiyo awamu inayohitaji fedha nyingi zaidi kuliko awamu

zilizopita. Makisio ya awali yanaonesha kuwa zitahitajika zaidi ya shilingi billion kumi

(10Billions) kukamilisha mradi huu kiasi ambacho ni kikubwa ukilinganisha na

takribani billion moja ambayo imekwishatumika kwa awamu ya I na awamu ya II.



Habari njema ni kwamba, mradi huu sasa utatengewa bajeti kubwa kwenye mwaka wa

fedha wa 2011/2012 ili ukamilike. Hii pia imepewa uzito na kauli ya Mh Waziri wa Maji

Jana tarehe 16/3/2011 kwenye uzinduzi wa wiki ya maji pale alipo thibitishia umma

kwa kusema, nanukuuu “ sasa tumedhamiria kuukamilisha mradi wa Bunda na

tutaukamilisha” mwisho wa kunukuu.


Hata hivyo mheshimiwa mgeni rasmi kazi za awali za maandalizi ya awamu hii ya tatu

zimeshaanza kufanyika kwani mhandisi mshauri ameshapatikana na anafanya kazi ya

kuandaa zabuni za ujenzi wa chujio, zabuni za ununuzi na utandazaji wa mabomba ya

maji, na anaandaa zabuni za uwekaji umeme wa msongo mkubwa na usimikaji wa

mitambo.


Mradi huu kwa ujumla unasimamiwa na Mamlaka ya Maji taka na Maji Safi Musoma

kwaniaba ya Wizara ya Maji na kwa upande wa Halmashauri wapo Mamlaka ya Maji

ya Bunda.


Mh. Mgeni Rasmi
Shughuli za awamu ya II ya mradi ambazo pamoja na kazi zingine ilihusisha ujenzi wa

tengi hili hapa tulipo kwenye Mlima Kaswaka, umechukua mwaka mmoja kutoka

tarehe 18/1/2009 hadi tarehe 31/12/2009 kwa gharamu ya Tsh. 226,567,000. Tengi

limejengwa kwa zege kali na nondo imara na limejengwa juu ya mwamba wa mawe ili

                                           4
kuwa imara muda wote. Tengi limejengwa na mkadarasi wa daraja la juu kabisa na

amelijengwa kwa kiwango bora kabisa na limejazwa maji na halivuji maji.



Naomba kurudia eneo hilo kwamba tengi letu ni imara wala halivuji maji na hivi sasa

lina maji yamo ndani ya tengi yamejaa na hayavuji hata kidogo.



Mh. Mgeni Rasmi
Pamoja na jitahada hizo zote hapo juu lakini Mamlaka ya Maji inachangamoto

mbalilmbali ambazo inakabiliana nazo, changamoto hizi ni;

     i. Miundimbinu ya maji inahujumiwa kwa bomba kutobolewa na wafugaji wa

          vijiji vya Guta, Tairo na Migungani

    ii. Uchakavu wa miundombinu ya maji hasa mabomba na mitambo

    iii. Kukatika nishati ya umeme mara kwa mara kumesababisha kuunguza pampu

          zetu za maji na vifaa vyake

    iv. Watumiaji maji kutolipa Ankara zao za maji kwa wakati

    v. Maji yanayosukumwa kutokidhi mahitaji ya jamii

    vi. Ukosefu wa fedha za kulipia Billi ya Umeme kwani ruzuku mara inakuja

          kidogo au miezi mingine ruzuku haiji kabisa na TANESCO hutishia kwa kutoa

          masaa 48 kuwa wasipolipwa bili yao watakata umeme kwenye mitambo yetu

          ya maji bila kujali kuwa Hospitali yetu ya wilaya (DDH) nayo itakosa maji

          ikiwa ni pamoja na wao wenyewe TANESCO watakosa maji

Hata hivyo Mamlaka ya maji Bunda ina mikakati kadhaa ili kukabiliana na changamoto

hizi. Mikakati yenyewe ni pamoja na;

      •    Ukamilshaji wa mradi mpya wa maji wenye chanzo chake Nyabehu

      •    Kuendelea ukarabati wa miundombinu ya maji kwa kutumia fedha kidogo

           tunazokusanya kwa wateja kila mwezi




                                            5
•     Ofisi ya Mkuu wa wilaya kusaidia namna ya kudhibiti hujuma na kwa

            Kutumia vyombo vya dola kama vile Mahakama, Polisi na serikali za Vijiji

            kusaidia kudhibiti hujuma dhidi ya miundombinu yetu

      •     Kuendelea kuiomba serikali kutoa fedha za ruzuku kwa wakati kama ilivyo

            kwenye bajeti ili shughuli zisikwame

Mh. Mgeni Rasmi
Hitimisho

Tunapenda kutoa rai kwa watumiaji maji kulipia Ankara zao za maji kwa wakati na

kuwaasa waepukane na utumiaji wa maji salama kwa Bustani, kuoshea magari n.k Pia

wasikubali kuchepusha maji yasipite kwenye mita kwani kwa kufanya hivyo ni kosa la

jinai na wanaweza kushitakiwa kwa mjibu wa sheria. Wananchi waisaidie Mamlaka

yao kufichua waovu wanaoihujumu Mamlaka isisonge mbele.


Mh. Mgeni Rasmi
Napenda pia kutumia nafasi hii kukushukuru wewe binafsi kwa kukubali mwaliko

wetu na kuwa nasi hapa leo. Pili niwashukuru kwa namna ya pekee wenzetu wa

Mamlaka ya Maji Bunda kwa kufanikisha shughuli hii ya uzindizi wa wiki ya Maji

hapa wilayani kwetu Bunda. Niwashukuru watumishi wa idara ya maji kwa ujumla na

kwa umoja na ushirikiano wao kufanikisha shughui hii na nawaomba waendelee hivyo

hivyo hadi tumalize Wiki ya Maji. Niwashukuru watumishi na wananchi waliofika

hapa na kwa namna ya pekee niwashukuru waandishi wa habari wa TV, Radio na

magazeti.

Maji ni Uhai na Usafi wa Mazingira ni Utu



Wiki ya Maji Oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee



Aksanteni kwa kunisikiliza

                                            6

Weitere ähnliche Inhalte

Was ist angesagt?

Lec 13 (Trickling Filters).pdf
Lec 13 (Trickling Filters).pdfLec 13 (Trickling Filters).pdf
Lec 13 (Trickling Filters).pdfMSaeed31
 
WATER RESOURCES PLANNING AND MANAGEMENT POSSIBILITIES IN CHAMARAJANAGAR TALUK...
WATER RESOURCES PLANNING AND MANAGEMENT POSSIBILITIES IN CHAMARAJANAGAR TALUK...WATER RESOURCES PLANNING AND MANAGEMENT POSSIBILITIES IN CHAMARAJANAGAR TALUK...
WATER RESOURCES PLANNING AND MANAGEMENT POSSIBILITIES IN CHAMARAJANAGAR TALUK...Prof. A.Balasubramanian
 
Tube-Wells and their Designs
Tube-Wells and their DesignsTube-Wells and their Designs
Tube-Wells and their DesignsAnand Kumar
 
Rain water harvesting in homes
Rain water  harvesting in homesRain water  harvesting in homes
Rain water harvesting in homesArvind Srinivasan
 
Improving Water Security in Water Stressed Bagmati River Basin, Nepal (2)
Improving Water Security in Water Stressed Bagmati River Basin, Nepal (2)Improving Water Security in Water Stressed Bagmati River Basin, Nepal (2)
Improving Water Security in Water Stressed Bagmati River Basin, Nepal (2)Oswar Mungkasa
 
Harokopio University & Library and Information Centre.History
Harokopio University & Library and Information Centre.History Harokopio University & Library and Information Centre.History
Harokopio University & Library and Information Centre.History Ifigenia Vardakosta
 
Individual responsibility in conservation of groundwater resources
Individual responsibility in conservation of groundwater resourcesIndividual responsibility in conservation of groundwater resources
Individual responsibility in conservation of groundwater resourcesAncy Varghese
 
Dam outlet works lecture 3
Dam outlet works lecture 3Dam outlet works lecture 3
Dam outlet works lecture 3Vidhi Khokhani
 
Sk reform presentation (from Akbayan Youth YiG Committee)
Sk reform presentation (from Akbayan Youth YiG Committee)Sk reform presentation (from Akbayan Youth YiG Committee)
Sk reform presentation (from Akbayan Youth YiG Committee)che-an
 
Water pollution in Dhaka City (Hatirjheel dhaka , bangladesh)
Water pollution in Dhaka City (Hatirjheel    dhaka , bangladesh)Water pollution in Dhaka City (Hatirjheel    dhaka , bangladesh)
Water pollution in Dhaka City (Hatirjheel dhaka , bangladesh)Ahsan Habib
 
Minor and micro irrigation
Minor and micro irrigationMinor and micro irrigation
Minor and micro irrigationGayatri Sherkar
 
Presentation_O_M.ppt
Presentation_O_M.pptPresentation_O_M.ppt
Presentation_O_M.pptsree886554
 
Training process manual for wtp narmada
Training  process manual for wtp narmadaTraining  process manual for wtp narmada
Training process manual for wtp narmadaAKHILESH AHIRWAL
 

Was ist angesagt? (20)

Lec 13 (Trickling Filters).pdf
Lec 13 (Trickling Filters).pdfLec 13 (Trickling Filters).pdf
Lec 13 (Trickling Filters).pdf
 
Canal design
Canal designCanal design
Canal design
 
Approaches for water sustainability
Approaches for water sustainabilityApproaches for water sustainability
Approaches for water sustainability
 
WATER RESOURCES PLANNING AND MANAGEMENT POSSIBILITIES IN CHAMARAJANAGAR TALUK...
WATER RESOURCES PLANNING AND MANAGEMENT POSSIBILITIES IN CHAMARAJANAGAR TALUK...WATER RESOURCES PLANNING AND MANAGEMENT POSSIBILITIES IN CHAMARAJANAGAR TALUK...
WATER RESOURCES PLANNING AND MANAGEMENT POSSIBILITIES IN CHAMARAJANAGAR TALUK...
 
Tube-Wells and their Designs
Tube-Wells and their DesignsTube-Wells and their Designs
Tube-Wells and their Designs
 
Rain water harvesting in homes
Rain water  harvesting in homesRain water  harvesting in homes
Rain water harvesting in homes
 
Improving Water Security in Water Stressed Bagmati River Basin, Nepal (2)
Improving Water Security in Water Stressed Bagmati River Basin, Nepal (2)Improving Water Security in Water Stressed Bagmati River Basin, Nepal (2)
Improving Water Security in Water Stressed Bagmati River Basin, Nepal (2)
 
Harokopio University & Library and Information Centre.History
Harokopio University & Library and Information Centre.History Harokopio University & Library and Information Centre.History
Harokopio University & Library and Information Centre.History
 
Water resource engineering project list 3
Water resource engineering project list  3Water resource engineering project list  3
Water resource engineering project list 3
 
Individual responsibility in conservation of groundwater resources
Individual responsibility in conservation of groundwater resourcesIndividual responsibility in conservation of groundwater resources
Individual responsibility in conservation of groundwater resources
 
SGLG110PDFTOPPT.pptx
SGLG110PDFTOPPT.pptxSGLG110PDFTOPPT.pptx
SGLG110PDFTOPPT.pptx
 
Dam outlet works lecture 3
Dam outlet works lecture 3Dam outlet works lecture 3
Dam outlet works lecture 3
 
Floating Bridge
Floating BridgeFloating Bridge
Floating Bridge
 
Sk reform presentation (from Akbayan Youth YiG Committee)
Sk reform presentation (from Akbayan Youth YiG Committee)Sk reform presentation (from Akbayan Youth YiG Committee)
Sk reform presentation (from Akbayan Youth YiG Committee)
 
Water pollution in Dhaka City (Hatirjheel dhaka , bangladesh)
Water pollution in Dhaka City (Hatirjheel    dhaka , bangladesh)Water pollution in Dhaka City (Hatirjheel    dhaka , bangladesh)
Water pollution in Dhaka City (Hatirjheel dhaka , bangladesh)
 
Sabarkantha District Profile
Sabarkantha District ProfileSabarkantha District Profile
Sabarkantha District Profile
 
Minor and micro irrigation
Minor and micro irrigationMinor and micro irrigation
Minor and micro irrigation
 
Earthwork
EarthworkEarthwork
Earthwork
 
Presentation_O_M.ppt
Presentation_O_M.pptPresentation_O_M.ppt
Presentation_O_M.ppt
 
Training process manual for wtp narmada
Training  process manual for wtp narmadaTraining  process manual for wtp narmada
Training process manual for wtp narmada
 

Andere mochten auch

Esl lead teacher october 30
Esl lead teacher october 30Esl lead teacher october 30
Esl lead teacher october 30shealyc
 
SCASA Anderson One Presentation
SCASA Anderson One PresentationSCASA Anderson One Presentation
SCASA Anderson One Presentationshealyc
 
Risala kwa wananchi kilele wiki ya maji 2013 bulendabufwe bunda iliyosomwa na...
Risala kwa wananchi kilele wiki ya maji 2013 bulendabufwe bunda iliyosomwa na...Risala kwa wananchi kilele wiki ya maji 2013 bulendabufwe bunda iliyosomwa na...
Risala kwa wananchi kilele wiki ya maji 2013 bulendabufwe bunda iliyosomwa na...Tanu Deule
 
White fang
White fangWhite fang
White fangflynt
 
Web usability
Web usabilityWeb usability
Web usabilitykhendai
 
White fang
White fangWhite fang
White fangflynt
 
Common bicycle project
Common bicycle project Common bicycle project
Common bicycle project Aykut Aysu
 
Scctm presentation
Scctm presentationScctm presentation
Scctm presentationshealyc
 

Andere mochten auch (16)

Esl lead teacher october 30
Esl lead teacher october 30Esl lead teacher october 30
Esl lead teacher october 30
 
Mp 8
Mp 8Mp 8
Mp 8
 
Tech deck animasyon
Tech deck animasyonTech deck animasyon
Tech deck animasyon
 
SCASA Anderson One Presentation
SCASA Anderson One PresentationSCASA Anderson One Presentation
SCASA Anderson One Presentation
 
Risala kwa wananchi kilele wiki ya maji 2013 bulendabufwe bunda iliyosomwa na...
Risala kwa wananchi kilele wiki ya maji 2013 bulendabufwe bunda iliyosomwa na...Risala kwa wananchi kilele wiki ya maji 2013 bulendabufwe bunda iliyosomwa na...
Risala kwa wananchi kilele wiki ya maji 2013 bulendabufwe bunda iliyosomwa na...
 
White fang
White fangWhite fang
White fang
 
La India
La IndiaLa India
La India
 
La India
La IndiaLa India
La India
 
Rogerio e dyovani gae
Rogerio e  dyovani gaeRogerio e  dyovani gae
Rogerio e dyovani gae
 
Mp 8
Mp 8Mp 8
Mp 8
 
Web usability
Web usabilityWeb usability
Web usability
 
White fang
White fangWhite fang
White fang
 
java programming
java programmingjava programming
java programming
 
2011 takvimi
2011 takvimi2011 takvimi
2011 takvimi
 
Common bicycle project
Common bicycle project Common bicycle project
Common bicycle project
 
Scctm presentation
Scctm presentationScctm presentation
Scctm presentation
 

Risala uzinduzi wiki ya maji bunda by Eng Deule Tanu

  • 1. Risala ya Uzinduzi wa Wiki ya Maji Wilayani Bunda iliyosomwa na Eng. Tanu Deule, Mhandisi wa maji wa wilaya ya Bunda kwenye Tengi la Maji la Mlima Kaswaka Bunda Mjini Tarehe 17 - Machi - 2011 Mh. Mgeni Rasmi (Mkuu wa Wilaya ya Bunda) Wah. Viongozi mliofika hapa (Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Bunda) Wafanyakazi wa Mamlaka ya Maji Bunda Wafanyakazi wenzangu wa Idara ya Maji kwa ujumla wenu Wafanyakazi wa Halmashauri yetu mliofika hapa kuungana nasi Ndugu zetu waandishi wa habari Ndugu Wananchi Mabibi na mabwana Tumsifu Yesu Kristo Asalaam Aleykum Bwana asifiwe Kabla ya yote napenda kumshukuru mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kutujalia uzima na leo tupo hapa Mh. Mgeni Rasmi Leo Halmashauri yetu inaungana na taifa zima kuadhimisha wiki ya maji ambayo imezinduliwa rasmi na Waziri wa Maji Mh. Prof Mark Mwandosya (MB) kwenye viwanja vya Nyamagana jijini Mwanza jana tarehe 16/3/2011. Wiki hii ya maji itahitimishwa tarehe 22/3/2011 ambayo ni siku ya Maji kidunia yaani World Water Day.
  • 2. Maadhimisho haya ya wiki ya maji ni ya 23 tangu yaanze kufanyika kitaifa mwaka 1988 na kauli mbiu ya mwaka huu ni “Maji kwaajili ya Miji: kukabiliana na changamoto mbalimbali Mijini” Mh. Mgeni Rasmi Miji inayotajwa kwenye kauli mbiu ya mwaka huu ni pamoja na mji wa Bunda. Na hii ndiyo maana Halmashauri yetu ya Wilaya Ikaonelea kuwa ni vema uzinduzi huu wa wiki ya maji kiwilaya ufanyike ndani ya viunga hivi vya Mjini na hasa kwenye mradi mpya wa maji Bunda Mjini. Mh. Mgeni Rasmi Kuhusu chombo chenye mamlaka ya kutoa huduma ya maji Bunda mjini Jukumu la utoaji huduma ya maji hapa Mjini, limekasimiwa kwa Mamlaka ya maji Bunda mjini yaani Bunda Water Supply Authority. Hii ni Mamlaka kamili iliyoanzishwa tarehe 21/6/2002 baada ya kutangazwa kwenye gazeti la serikali. Bodi yake ya kwanza ilianza kutenda kazi tarehe 1Juni 2003 na hivi sasa kuna Bodi ya 3 iliyoteuliwa rasmi tarehe 10 januari mwaka huu wa 2011. Mh. Mgeni Rasmi Kuhusu huduma ya maji hapa mjini. • Kiwango cha maji yanayozalishwa kwa siku yameongezeka kutoka lita 720,000 mwaka 2006 hadi liata 1,260,000 mwaka 2010 • Wateja wameongezeka kutoka 650 mwaka 2006 hadi wateja1,227 mwaka 2010 • Wastani wa watu wenye maji ya bomba wameongezeka kutoka asilimia 15.4 mwaka 2006 hadi asilimia 27.4 mwaka 2010 Mh. Mgeni Rasmi Kuhusu mradi Mpya wa Maji Bunda Mjini 2
  • 3. Takwimu iliyoonyeshwa hapo juu kwamba katika watu 100 ni watu 27 tu ndo wanapata maji ya bomba inadhihirisha ukubwa wa tatizo lililopo na kwamba changamoto hii ni kubwa sana kwetu. Hivyo basi, Halmashauri kwa kushirikiana na Wizara ya Maji na kwa Msukumo wa pekee wa mheshimiwa Mbunge wa jimbo la Bunda, Mh. Stephen M. Wasira (MB) na Waziri wa nchi ofisi ya raisi –Mawasiliano na Uratibu, tumeanza kutekeleza mradi mpya wa maji hapa Bunda mjini utakaokuwa na chanzo chake kwenye kijiji cha Nyabehu kilichopo umbali wa kilomita 26 kutoka hapa mjini. Mradi huu ni mkubwa sana ukiangalia gharama zake hadi hapo utakapo kamilika, na utaona kuwa umekuwa ukitengewa fedha kidogo hadi kupelekea utekelezwe kwa awamu kadiri fedha zilivyokuwa zinapatikana, kwani kusubiri fedha hadi zitimie zote ndiyo mradi uanze kujengwa haukuonekana kuwa ni uamuzi mzuri. Kwa fedha zilizokuwa zinapatikana, mradi huu umetekelezwa kama ifuatavyo; Awamu ya I: Zimenunuliwa pampu mpya 9 za kusukuma maji na tayari zipo hapa Wilayani Bunda zimetunzwa kwenye Bohari yetu Awamu ya II: Umefanyika ujenzi wa i. Tengi la maji Migungani lenye ujazo wa lita 225,000 ii. Tengi la kwenye Mlima Kaswaka lenye ujazo wa lita 675,000 iii. Nyumba ya kufunga pampu (Pump House) iv. Nyumba ya wahudumu wa pamp (pump attendant house) na choo yake v. Barabara ya kwenda kwenye tengi la maji kwenye Mlima Kaswaka Awamu ya II: Awamu hii bado haijatekelezwa lakini itahusisha kazi zifuatazo • Ujenzi wa chujio (treatment plant) • Kununua na kulaza mabomba ya bomba kuu kilometa 26 • Kusimika pampu 3
  • 4. Kuingiza umeme wenye msongo mkubwa, na • Kusuka mtandao mpya wa usambazaji maji hapa mjini Mh. Mgeni Rasmi Awamu hii ya tatu ndiyo awamu inayohitaji fedha nyingi zaidi kuliko awamu zilizopita. Makisio ya awali yanaonesha kuwa zitahitajika zaidi ya shilingi billion kumi (10Billions) kukamilisha mradi huu kiasi ambacho ni kikubwa ukilinganisha na takribani billion moja ambayo imekwishatumika kwa awamu ya I na awamu ya II. Habari njema ni kwamba, mradi huu sasa utatengewa bajeti kubwa kwenye mwaka wa fedha wa 2011/2012 ili ukamilike. Hii pia imepewa uzito na kauli ya Mh Waziri wa Maji Jana tarehe 16/3/2011 kwenye uzinduzi wa wiki ya maji pale alipo thibitishia umma kwa kusema, nanukuuu “ sasa tumedhamiria kuukamilisha mradi wa Bunda na tutaukamilisha” mwisho wa kunukuu. Hata hivyo mheshimiwa mgeni rasmi kazi za awali za maandalizi ya awamu hii ya tatu zimeshaanza kufanyika kwani mhandisi mshauri ameshapatikana na anafanya kazi ya kuandaa zabuni za ujenzi wa chujio, zabuni za ununuzi na utandazaji wa mabomba ya maji, na anaandaa zabuni za uwekaji umeme wa msongo mkubwa na usimikaji wa mitambo. Mradi huu kwa ujumla unasimamiwa na Mamlaka ya Maji taka na Maji Safi Musoma kwaniaba ya Wizara ya Maji na kwa upande wa Halmashauri wapo Mamlaka ya Maji ya Bunda. Mh. Mgeni Rasmi Shughuli za awamu ya II ya mradi ambazo pamoja na kazi zingine ilihusisha ujenzi wa tengi hili hapa tulipo kwenye Mlima Kaswaka, umechukua mwaka mmoja kutoka tarehe 18/1/2009 hadi tarehe 31/12/2009 kwa gharamu ya Tsh. 226,567,000. Tengi limejengwa kwa zege kali na nondo imara na limejengwa juu ya mwamba wa mawe ili 4
  • 5. kuwa imara muda wote. Tengi limejengwa na mkadarasi wa daraja la juu kabisa na amelijengwa kwa kiwango bora kabisa na limejazwa maji na halivuji maji. Naomba kurudia eneo hilo kwamba tengi letu ni imara wala halivuji maji na hivi sasa lina maji yamo ndani ya tengi yamejaa na hayavuji hata kidogo. Mh. Mgeni Rasmi Pamoja na jitahada hizo zote hapo juu lakini Mamlaka ya Maji inachangamoto mbalilmbali ambazo inakabiliana nazo, changamoto hizi ni; i. Miundimbinu ya maji inahujumiwa kwa bomba kutobolewa na wafugaji wa vijiji vya Guta, Tairo na Migungani ii. Uchakavu wa miundombinu ya maji hasa mabomba na mitambo iii. Kukatika nishati ya umeme mara kwa mara kumesababisha kuunguza pampu zetu za maji na vifaa vyake iv. Watumiaji maji kutolipa Ankara zao za maji kwa wakati v. Maji yanayosukumwa kutokidhi mahitaji ya jamii vi. Ukosefu wa fedha za kulipia Billi ya Umeme kwani ruzuku mara inakuja kidogo au miezi mingine ruzuku haiji kabisa na TANESCO hutishia kwa kutoa masaa 48 kuwa wasipolipwa bili yao watakata umeme kwenye mitambo yetu ya maji bila kujali kuwa Hospitali yetu ya wilaya (DDH) nayo itakosa maji ikiwa ni pamoja na wao wenyewe TANESCO watakosa maji Hata hivyo Mamlaka ya maji Bunda ina mikakati kadhaa ili kukabiliana na changamoto hizi. Mikakati yenyewe ni pamoja na; • Ukamilshaji wa mradi mpya wa maji wenye chanzo chake Nyabehu • Kuendelea ukarabati wa miundombinu ya maji kwa kutumia fedha kidogo tunazokusanya kwa wateja kila mwezi 5
  • 6. Ofisi ya Mkuu wa wilaya kusaidia namna ya kudhibiti hujuma na kwa Kutumia vyombo vya dola kama vile Mahakama, Polisi na serikali za Vijiji kusaidia kudhibiti hujuma dhidi ya miundombinu yetu • Kuendelea kuiomba serikali kutoa fedha za ruzuku kwa wakati kama ilivyo kwenye bajeti ili shughuli zisikwame Mh. Mgeni Rasmi Hitimisho Tunapenda kutoa rai kwa watumiaji maji kulipia Ankara zao za maji kwa wakati na kuwaasa waepukane na utumiaji wa maji salama kwa Bustani, kuoshea magari n.k Pia wasikubali kuchepusha maji yasipite kwenye mita kwani kwa kufanya hivyo ni kosa la jinai na wanaweza kushitakiwa kwa mjibu wa sheria. Wananchi waisaidie Mamlaka yao kufichua waovu wanaoihujumu Mamlaka isisonge mbele. Mh. Mgeni Rasmi Napenda pia kutumia nafasi hii kukushukuru wewe binafsi kwa kukubali mwaliko wetu na kuwa nasi hapa leo. Pili niwashukuru kwa namna ya pekee wenzetu wa Mamlaka ya Maji Bunda kwa kufanikisha shughuli hii ya uzindizi wa wiki ya Maji hapa wilayani kwetu Bunda. Niwashukuru watumishi wa idara ya maji kwa ujumla na kwa umoja na ushirikiano wao kufanikisha shughui hii na nawaomba waendelee hivyo hivyo hadi tumalize Wiki ya Maji. Niwashukuru watumishi na wananchi waliofika hapa na kwa namna ya pekee niwashukuru waandishi wa habari wa TV, Radio na magazeti. Maji ni Uhai na Usafi wa Mazingira ni Utu Wiki ya Maji Oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee Aksanteni kwa kunisikiliza 6