SlideShare ist ein Scribd-Unternehmen logo
1 von 4
UMUHIMU WA KUJIFUNZA NADHARIA ZA FONOLOJIA


UTANGULIZI
Kila linalofanywa na binadamu ili liwe ni lenye kufanikiwa linahitaji mwongozo ambao
utakuwa dira kwa jambo hilo. Mwongozo wa jambo lolote sharti uwe na vigezo ambavyo
vitawawezesha watu wengine kujifunza na kulifahamu jambo hilo. Kutokana na vigezo
hivyo, huwajengea utaratibu maalumu unaowawezesha na kuainisha ubora na udhaifu
unaojitokea katika jambo hilo.


Lengo la kazi hii ni kueleza umuhimu wa kujifunza nadharia mbali mbali za fonolojia.
Lakini kabla hatujajikita katika kiini cha swali ni vyema tukajikumbusha fasili ya
nadharia, ambapo neno hili ni istilahi ya msingi katika swali letu. Kwa mujibu wa
Massamba, D.P.B (2004:63) Nadharia ni kanuni na misingi ambayo hujengwa katika
muundo wa kimawazo kwa madhumuni ya kutumiwa kama kiolezo ya kueleza jambo.


Kwa mujibu wa fasili hiyo, tunapozungumzia neno nadharia tuna maana kwamba
nadharia ni maelezo ya jambo yaliyofungamana na vigezo vilivyowekwa au
vilivyozalishwa kutokana na uchunguzi uliofanywa. Vigezo hivyo ndivyo vinavyounda
kanuni na misingi ya kulieleza jambo lilokusudiwa. Nadharia kama mawazo, inaweza
kutokana na mtaalamu au kundi la wataalamu waliokaa na kufanya uchunguzi juu ya
jambo fulani.


Nadharia za fonolojia kwa ujumla wake ni mawazo ya wanaisimu kuhusu fonolojia za
lugha yaliyofungamana vigezo vilivyowekwa na wataalamu hao baada ya kufanya
uchunguzi. Nadharia za fonolojia ni mwongozo unaomwelekeza mwanaisimu chipukizi
au mtu anayejifundisha fonolojia, kuifahamu fonolojia ya lugha katika vipengele vyake
vyote.   Kupitia   mwongozo      huu,   mwanaisimu   hujijengea   utaratibu   maalumu
utakaomwezesha kujua ubora na udhaifu utakaojitokeza katika nadharia nyengine.


UMUHIMU WA KUJIFUNZA NADHARIA ZA FONOLOJIA




                                           1
Fonolojia kama tawi la isimu ni kongwe sana. Limeanza kufanyiwa kazi katika karne
nyingi zilizopita. Maendeleo hayo ya fonolojia yanaonesha kupita katika hatua kadhaa,
hatua ambazo zimejengwa kwa nadharia tofauti. Hivyo basi, kujifunza nadharia mbali
mbali za fonolojia ni muhimu kama ifuatavyo:-


Mosi, taaluma za fonolojia ni muhimu sana katika jamii yoyote ya lugha. Tawi hili la
isimu hujishughulisha na uchunguzi na uchanganuzi wa sauti za lugha kisayansi.
Kutokana na umuhimu wa taaluma hii kwa jamii hatuwezi kuibeza. Njia mwafaka ya
zaidi ya kushughulikia somo la fonolojia kitaalamu ni kutumia nadharia. Hivyo kujifunza
nadharia ni muhimu kwa sababu tunapata kujua maumbile ya lugha tofauti ulimwenguni.
Mfano tunaweza kujua makundi ya lugha kama vile lugha zenye toni asilia, lugha zenye
viini toni, lugha zenye mkazo na lugha ambazo hazina toni wala mkazo.


Pili, nadharia za fonolojia humsaidia na kumuongoza mwanaisimu kuzibainisha kadhia
mbali mbali zinazozikabili kazi za wanaisimu wengine. Mfano, wanaisimu; Noam
Chomsky na Morris Halle walisoma kazi za fonolojia zilizoandikwa na akina Ferdinand
de Saussure, Bloomfield na wengine na kuona kuwa wanaisimu hao walitofautiana katika
kuzieleza sauti za lugha licha ya kuwa walieleza kitu kimoja. Kwa hivyo, Chomsky na
Halle wakaanzisha nadharia iliyojulikana kama Fonolojia Zalishi ili kujaribu kutatua
matatizo hayo.


Tatu, kujifunza nadharia mbali mbali za fonolojia huwasaidia wanaisimu chipukizi kuwa
mahiri na weledi katika uwanja wa fonolojia. Kwa sababu nadharia zinatoa mwongozo
unaowaelekeza wanaisimu kujua hatua mbali mbali za maendeleo zilizopitiwa katika
uwanja wa fonolojia. Kutokana na kujifunza nadharia mbali mbali mwanaisimu hupata
vigezo imara vinavyosaidia kutanua taaluma na maarifa aliyoyapata katika uwanja huu
wa fonolojia.


Nne, ni kawaida ya binadamu kudadisi kazi za wengine ili kuweka bayana ubora na
udhaifu wa uliomo katika kazi hiyo hasa inapokabiliwa na hali tete. Katika hali ya kuzua,
kuchuja na kukuza mikakati ya kutafitia , nadharia mpya inahitajika ili kuzilinda hoja



                                           2
zake. Mfano, katika uwanja wa fonolojia, mwanaisimu John Goldsmith ilitafiti kazi ya
Fonolojia Zalishi iliyoandikwa na Chomsky na Halle na kubaini kuwa yapo matatizo
kadhaa yanayojitokeza wakati wa kuwakilisha vipambasauti kama vile mkazo, toni,
usilabi na unazali kwani vipengele vyote vya kifonolojia viliwakilishwa kwa mstari
mlalo. Ili kujaribu kutatua matatizo hayo, Goldsmith akanzisha nadharia mpya
iliyojulikana kama Fonolojia ya Vipandesauti Huru. Nadharia yake ilipendekeza
vipambasauti viwakilishwe kwa mistari mingi.


Tano, kujifunza nadharia mbali mbali za fonolojia ni muhimu kwa sababu hutuwezesha
kujua historia na maendeleo ya fonolojia katika vipengele mbali mbali. Kwa mfano
tunapata kuzijua nadharia za awali na waasisi wake. Matatizo yaliyojitokeza katika
nadharia hizo pamoja na kuzijua nadharia za sasa na namna zinavyojaribu kutatua
matatizo yaliyojitokeza katika nadharia za zamani. Mfano, kupitia nadharia za zamani
tunamjua mwanaisimu Trubetzkoy ambaye alianzisha nadharia ya fonimu. Wanaisimu
wengi wa sasa hawakubaliani na nadharia yake lakini hawawezi kuubeza mchango wake
katika maendeleo ya nadharia za fonolojia na sayansi ya isimu.


Kutokana na maelezo hayo, tunaweza kusema kuwa kujifunza nadharia mbali mbali za
fonolojia ni muhimu sana kwa wanafunzi wa lugha, wanaisimu na watumiaji wengine wa
lugha. kwa lengo la kubaini ubora na udhaifu wa nadharia ili tuweze kuzitumia nadharia
hizo kuchunguza, kuchambua na kuchanganua vipengele mbalimbali vya fonolojia.
Mwanaisimu anaejua nadharia mbali mbali za fonolojia huwa mahiri na mjuzi aliyebobea
katika kuvichambua vipengele mbali mbali vya fonolojia.


Pamoja na hakuna nadharia inayojitosheleza katika kiunzi chake. Hii ina maana kwamba
tunazo nadharia mbali mbali zinazohusu taaluma hii ya fonolojia lakini kila nadharia ina
ubora wake na udhaifu wake. Hivyo wanaisimu waendelee kufanya tafiti ili kuunda
nadharia mpya.
                                      MAREJEO
Massamba,D.P.B (2004), Kamusi ya Falsafa ya Lugha na Isimu. Dar es Salaam
                 University Press.



                                           3
Massamba,D.P.B (1996), Phonological Theory, History and Development, Dar es Salaam
               University Press.




                                        4

Weitere ähnliche Inhalte

Was ist angesagt?

Ling101 phonological rules
Ling101 phonological rulesLing101 phonological rules
Ling101 phonological rules
minhanviet
 
Allophone and phoneme. persentation
Allophone and phoneme. persentationAllophone and phoneme. persentation
Allophone and phoneme. persentation
Dessy Restu Restu
 

Was ist angesagt? (20)

Comprehension theory
Comprehension theoryComprehension theory
Comprehension theory
 
Origin of Language
 Origin of Language Origin of Language
Origin of Language
 
Characteristics and features of Language
Characteristics and features of Language Characteristics and features of Language
Characteristics and features of Language
 
Tamthilia ni nini?
Tamthilia ni nini?Tamthilia ni nini?
Tamthilia ni nini?
 
Linguistics the sound patterns of language
Linguistics  the sound patterns of languageLinguistics  the sound patterns of language
Linguistics the sound patterns of language
 
Ling101 phonological rules
Ling101 phonological rulesLing101 phonological rules
Ling101 phonological rules
 
MATUMIZI YA SARUFI
MATUMIZI YA SARUFIMATUMIZI YA SARUFI
MATUMIZI YA SARUFI
 
LAD
LADLAD
LAD
 
Mofolojia
MofolojiaMofolojia
Mofolojia
 
Theories in Language Description
Theories in Language DescriptionTheories in Language Description
Theories in Language Description
 
Chomsky’s Universal Grammar
Chomsky’s Universal GrammarChomsky’s Universal Grammar
Chomsky’s Universal Grammar
 
Characteristics of language.ppt
Characteristics of language.pptCharacteristics of language.ppt
Characteristics of language.ppt
 
Allophone and phoneme. persentation
Allophone and phoneme. persentationAllophone and phoneme. persentation
Allophone and phoneme. persentation
 
Chimbuko na Asili ya Kiswahili
Chimbuko na Asili ya KiswahiliChimbuko na Asili ya Kiswahili
Chimbuko na Asili ya Kiswahili
 
Discourse Analysis
Discourse AnalysisDiscourse Analysis
Discourse Analysis
 
Tafsiri na ukalimani
Tafsiri na ukalimaniTafsiri na ukalimani
Tafsiri na ukalimani
 
Noam Chomsky
Noam ChomskyNoam Chomsky
Noam Chomsky
 
Ethnolinguistic
EthnolinguisticEthnolinguistic
Ethnolinguistic
 
Corpus linguistics
Corpus linguisticsCorpus linguistics
Corpus linguistics
 
Roman jakobson linguistic
Roman jakobson linguisticRoman jakobson linguistic
Roman jakobson linguistic
 

Andere mochten auch

The importance of morphology and syntax in the formation as teachers
The importance of morphology and syntax in the formation as teachersThe importance of morphology and syntax in the formation as teachers
The importance of morphology and syntax in the formation as teachers
Percy Cosme
 
Waraka wa elimu na. 4 wa mwaka 2014 kuhusu utayarishaji wa vifaa vya kujifunz...
Waraka wa elimu na. 4 wa mwaka 2014 kuhusu utayarishaji wa vifaa vya kujifunz...Waraka wa elimu na. 4 wa mwaka 2014 kuhusu utayarishaji wa vifaa vya kujifunz...
Waraka wa elimu na. 4 wa mwaka 2014 kuhusu utayarishaji wa vifaa vya kujifunz...
elimutanzania
 
Definition of phonology
Definition of phonologyDefinition of phonology
Definition of phonology
Javico Suarez
 
MAFUNZO YA UJASIRIAMALI
MAFUNZO YA UJASIRIAMALIMAFUNZO YA UJASIRIAMALI
MAFUNZO YA UJASIRIAMALI
Kaka Sule
 
The Important of Phonetics in English Language Learning
The Important of Phonetics in English Language LearningThe Important of Phonetics in English Language Learning
The Important of Phonetics in English Language Learning
maaj809
 
Morphemes
MorphemesMorphemes
Morphemes
moniozy
 
A comparison of german and english –
A comparison of german and english –A comparison of german and english –
A comparison of german and english –
Lauri Rintelman
 

Andere mochten auch (18)

Maana ya maana!
Maana ya maana!Maana ya maana!
Maana ya maana!
 
The importance of morphology and syntax in the formation as teachers
The importance of morphology and syntax in the formation as teachersThe importance of morphology and syntax in the formation as teachers
The importance of morphology and syntax in the formation as teachers
 
UTAFITI WA KIELIMU
UTAFITI  WA KIELIMUUTAFITI  WA KIELIMU
UTAFITI WA KIELIMU
 
Lahaja za kiswahili kwa ujumla
Lahaja za kiswahili kwa ujumlaLahaja za kiswahili kwa ujumla
Lahaja za kiswahili kwa ujumla
 
Waraka wa elimu na. 4 wa mwaka 2014 kuhusu utayarishaji wa vifaa vya kujifunz...
Waraka wa elimu na. 4 wa mwaka 2014 kuhusu utayarishaji wa vifaa vya kujifunz...Waraka wa elimu na. 4 wa mwaka 2014 kuhusu utayarishaji wa vifaa vya kujifunz...
Waraka wa elimu na. 4 wa mwaka 2014 kuhusu utayarishaji wa vifaa vya kujifunz...
 
Semantiki
SemantikiSemantiki
Semantiki
 
Rm 211
Rm 211Rm 211
Rm 211
 
CHIMBUKO LA FASIHI
CHIMBUKO LA FASIHICHIMBUKO LA FASIHI
CHIMBUKO LA FASIHI
 
Importance of phonology
Importance of phonologyImportance of phonology
Importance of phonology
 
JEDWALI LA KUTAHINI
JEDWALI LA KUTAHINIJEDWALI LA KUTAHINI
JEDWALI LA KUTAHINI
 
Definition of phonology
Definition of phonologyDefinition of phonology
Definition of phonology
 
Jipime Sayansi Darasa la Sita
Jipime Sayansi Darasa la SitaJipime Sayansi Darasa la Sita
Jipime Sayansi Darasa la Sita
 
MAFUNZO YA UJASIRIAMALI
MAFUNZO YA UJASIRIAMALIMAFUNZO YA UJASIRIAMALI
MAFUNZO YA UJASIRIAMALI
 
The Important of Phonetics in English Language Learning
The Important of Phonetics in English Language LearningThe Important of Phonetics in English Language Learning
The Important of Phonetics in English Language Learning
 
Axiology
AxiologyAxiology
Axiology
 
Morphemes
MorphemesMorphemes
Morphemes
 
How To Make Time For A Side Hustle
How To Make Time For A Side HustleHow To Make Time For A Side Hustle
How To Make Time For A Side Hustle
 
A comparison of german and english –
A comparison of german and english –A comparison of german and english –
A comparison of german and english –
 

Umuhimu wa kujifunza nadharia za fonolojia

  • 1. UMUHIMU WA KUJIFUNZA NADHARIA ZA FONOLOJIA UTANGULIZI Kila linalofanywa na binadamu ili liwe ni lenye kufanikiwa linahitaji mwongozo ambao utakuwa dira kwa jambo hilo. Mwongozo wa jambo lolote sharti uwe na vigezo ambavyo vitawawezesha watu wengine kujifunza na kulifahamu jambo hilo. Kutokana na vigezo hivyo, huwajengea utaratibu maalumu unaowawezesha na kuainisha ubora na udhaifu unaojitokea katika jambo hilo. Lengo la kazi hii ni kueleza umuhimu wa kujifunza nadharia mbali mbali za fonolojia. Lakini kabla hatujajikita katika kiini cha swali ni vyema tukajikumbusha fasili ya nadharia, ambapo neno hili ni istilahi ya msingi katika swali letu. Kwa mujibu wa Massamba, D.P.B (2004:63) Nadharia ni kanuni na misingi ambayo hujengwa katika muundo wa kimawazo kwa madhumuni ya kutumiwa kama kiolezo ya kueleza jambo. Kwa mujibu wa fasili hiyo, tunapozungumzia neno nadharia tuna maana kwamba nadharia ni maelezo ya jambo yaliyofungamana na vigezo vilivyowekwa au vilivyozalishwa kutokana na uchunguzi uliofanywa. Vigezo hivyo ndivyo vinavyounda kanuni na misingi ya kulieleza jambo lilokusudiwa. Nadharia kama mawazo, inaweza kutokana na mtaalamu au kundi la wataalamu waliokaa na kufanya uchunguzi juu ya jambo fulani. Nadharia za fonolojia kwa ujumla wake ni mawazo ya wanaisimu kuhusu fonolojia za lugha yaliyofungamana vigezo vilivyowekwa na wataalamu hao baada ya kufanya uchunguzi. Nadharia za fonolojia ni mwongozo unaomwelekeza mwanaisimu chipukizi au mtu anayejifundisha fonolojia, kuifahamu fonolojia ya lugha katika vipengele vyake vyote. Kupitia mwongozo huu, mwanaisimu hujijengea utaratibu maalumu utakaomwezesha kujua ubora na udhaifu utakaojitokeza katika nadharia nyengine. UMUHIMU WA KUJIFUNZA NADHARIA ZA FONOLOJIA 1
  • 2. Fonolojia kama tawi la isimu ni kongwe sana. Limeanza kufanyiwa kazi katika karne nyingi zilizopita. Maendeleo hayo ya fonolojia yanaonesha kupita katika hatua kadhaa, hatua ambazo zimejengwa kwa nadharia tofauti. Hivyo basi, kujifunza nadharia mbali mbali za fonolojia ni muhimu kama ifuatavyo:- Mosi, taaluma za fonolojia ni muhimu sana katika jamii yoyote ya lugha. Tawi hili la isimu hujishughulisha na uchunguzi na uchanganuzi wa sauti za lugha kisayansi. Kutokana na umuhimu wa taaluma hii kwa jamii hatuwezi kuibeza. Njia mwafaka ya zaidi ya kushughulikia somo la fonolojia kitaalamu ni kutumia nadharia. Hivyo kujifunza nadharia ni muhimu kwa sababu tunapata kujua maumbile ya lugha tofauti ulimwenguni. Mfano tunaweza kujua makundi ya lugha kama vile lugha zenye toni asilia, lugha zenye viini toni, lugha zenye mkazo na lugha ambazo hazina toni wala mkazo. Pili, nadharia za fonolojia humsaidia na kumuongoza mwanaisimu kuzibainisha kadhia mbali mbali zinazozikabili kazi za wanaisimu wengine. Mfano, wanaisimu; Noam Chomsky na Morris Halle walisoma kazi za fonolojia zilizoandikwa na akina Ferdinand de Saussure, Bloomfield na wengine na kuona kuwa wanaisimu hao walitofautiana katika kuzieleza sauti za lugha licha ya kuwa walieleza kitu kimoja. Kwa hivyo, Chomsky na Halle wakaanzisha nadharia iliyojulikana kama Fonolojia Zalishi ili kujaribu kutatua matatizo hayo. Tatu, kujifunza nadharia mbali mbali za fonolojia huwasaidia wanaisimu chipukizi kuwa mahiri na weledi katika uwanja wa fonolojia. Kwa sababu nadharia zinatoa mwongozo unaowaelekeza wanaisimu kujua hatua mbali mbali za maendeleo zilizopitiwa katika uwanja wa fonolojia. Kutokana na kujifunza nadharia mbali mbali mwanaisimu hupata vigezo imara vinavyosaidia kutanua taaluma na maarifa aliyoyapata katika uwanja huu wa fonolojia. Nne, ni kawaida ya binadamu kudadisi kazi za wengine ili kuweka bayana ubora na udhaifu wa uliomo katika kazi hiyo hasa inapokabiliwa na hali tete. Katika hali ya kuzua, kuchuja na kukuza mikakati ya kutafitia , nadharia mpya inahitajika ili kuzilinda hoja 2
  • 3. zake. Mfano, katika uwanja wa fonolojia, mwanaisimu John Goldsmith ilitafiti kazi ya Fonolojia Zalishi iliyoandikwa na Chomsky na Halle na kubaini kuwa yapo matatizo kadhaa yanayojitokeza wakati wa kuwakilisha vipambasauti kama vile mkazo, toni, usilabi na unazali kwani vipengele vyote vya kifonolojia viliwakilishwa kwa mstari mlalo. Ili kujaribu kutatua matatizo hayo, Goldsmith akanzisha nadharia mpya iliyojulikana kama Fonolojia ya Vipandesauti Huru. Nadharia yake ilipendekeza vipambasauti viwakilishwe kwa mistari mingi. Tano, kujifunza nadharia mbali mbali za fonolojia ni muhimu kwa sababu hutuwezesha kujua historia na maendeleo ya fonolojia katika vipengele mbali mbali. Kwa mfano tunapata kuzijua nadharia za awali na waasisi wake. Matatizo yaliyojitokeza katika nadharia hizo pamoja na kuzijua nadharia za sasa na namna zinavyojaribu kutatua matatizo yaliyojitokeza katika nadharia za zamani. Mfano, kupitia nadharia za zamani tunamjua mwanaisimu Trubetzkoy ambaye alianzisha nadharia ya fonimu. Wanaisimu wengi wa sasa hawakubaliani na nadharia yake lakini hawawezi kuubeza mchango wake katika maendeleo ya nadharia za fonolojia na sayansi ya isimu. Kutokana na maelezo hayo, tunaweza kusema kuwa kujifunza nadharia mbali mbali za fonolojia ni muhimu sana kwa wanafunzi wa lugha, wanaisimu na watumiaji wengine wa lugha. kwa lengo la kubaini ubora na udhaifu wa nadharia ili tuweze kuzitumia nadharia hizo kuchunguza, kuchambua na kuchanganua vipengele mbalimbali vya fonolojia. Mwanaisimu anaejua nadharia mbali mbali za fonolojia huwa mahiri na mjuzi aliyebobea katika kuvichambua vipengele mbali mbali vya fonolojia. Pamoja na hakuna nadharia inayojitosheleza katika kiunzi chake. Hii ina maana kwamba tunazo nadharia mbali mbali zinazohusu taaluma hii ya fonolojia lakini kila nadharia ina ubora wake na udhaifu wake. Hivyo wanaisimu waendelee kufanya tafiti ili kuunda nadharia mpya. MAREJEO Massamba,D.P.B (2004), Kamusi ya Falsafa ya Lugha na Isimu. Dar es Salaam University Press. 3
  • 4. Massamba,D.P.B (1996), Phonological Theory, History and Development, Dar es Salaam University Press. 4