Beginners Guide to TikTok for Search - Rachel Pearson - We are Tilt __ Bright...
Zumm A4 Leaflet - Swahili
1. Zungumza na Mtoto Mchanga
Talk to Your Baby
Taarifa ya Utafiti na Ujuzi Uliotokana na Utafiti
2013 – 2015
Wakusanya taarifa wakijifunza jinsi ya kutumia
Kipimo cha Uelewa wa Lugha.
Baba huyu alihudhuria mafunzo ya kujengewa uwezo pasipo kudhamiria, lakini sasa anajisikia
kuona fahari kwa ajili ya mwanae, na akaondoka akiwa amembeba huku wakiendelea kuongea.
Angalia tofauti kati ya mama na mtoto baada ya saa moja tu ya
mafunzo kuhusu jinsi ya kuzungumza na mwanae mchanga.
2 Page Folder Leaflet A4 Swahili version.indd 1 01/12/2015 08:29
2. Zungumza na Mtoto Mchanga
Mambo ya Msingi wa jambo hili
Mfumo wa Utafiti
Upoushahidiwenyenguvukimataifakuhusiananasualalaumuhimu
wa mazingira yenye tija ya kukuza vipaji vya lugha katika mwaka
wa kwanza wa uhai wa mtoto. Watoto wanaozungumzishwa sana
kwa njia sahihi tangu wanapozaliwa hujifunza kuongea mapema,
piakuongeavyema. Watoto,wanaojuanakuelewamanenomengi
na kuongea mapema wana uelekeo wa kupata mafanikio katika
kujifunza kusoma na kuandika pindi wapelekwapo shuleni.
Ushahidi wa yale watu waliyotuambia kwa upande mmoja, na
mitazamo ya wana taaluma wenzetu kwa upande mwingine,
pamoja na yale tuliyoweza kuyabaini katika medani za utafiti,
yote haya yanachangia kubainisha kwamba mazingira ya uelewa
wa lugha kwa watoto wa Kitanzania si ya kiwango cha juu sana
kwa kadiri ilivyopaswa iwe. Ni kana kwamba kwa jumla, wazazi
hawazungumzi sana na watoto wao wawapo bado wachanga na
wala hawajui umuhimu wa kulifanya jambo hili.
Kundi la washika dau takribani 24 kutoka Serikalini pamoja na
wadau wengine wa maendeleo walikutana mwishoni mwa mwaka
2011 ili kuamua ni nini kifanyike; na hapo ndipo ilipoamliwa
kwamba hatua ya kwanza itakuwa ni kufanya utafiti wa kitaalamu.
Huu ni utafiti wa kwanza wa mazingira ya lugha kwa watoto
wachanga katika nchi za Kiafrika zilizo kusini ya jangwa la Sahara.
Maswali ambayo utafiti huu ulilenga kuyatafutia majibu yalikuwa
kama ifuatavyo:
• ‘Mazingira ya lugha kwa watoto wachanga nchini Tanzania
hasa katika mwaka wa kwanza wa uhai wao yakoje?’
• ‘Ni kwa njia gani, kama inawezekana, mazingira ya lugha kwa
watoto wachanga yaboreshwe, kwa namna itakayoongeza
uwezo wa kielimu kwa watoto wachanga na hatimaye watoto
kwa jumla?’
Mnamo mwaka 2012, utafiti wa awali ulifanyika katika wilaya za
Moshi vijijini na visiwa vya Chole na Mafia. UBS Optimus, ambayo
ni wakfu wa banki katika nchi ya Switzerland ulitoa fuko la fedha
lililotosheleza kufanyika utafiti katika maeneo makubwa, na
kwa hiyo malengo ya utafiti yaliboreshwa kutokana na matokeo
ya utafiti wa awali. Kibali kutoka COSTECH kilitolewa mwaka
2013, ili utafiti wa majaribio ufanyike katika kaya takriban 1,000
kutoka katika Wilaya tano zilizopatikana kwa kubahatisha pasi na
kuzingatia vigezo vyovyote.
Mfumo wa utafiti waweza kuonekana katika Jedwali 1. Watafiti wasaidizi wa Kitanzania walikusanya taarifa kutoka katika mazingira ya
ndaniyakaya,waalimukatikamaeneoutafitiulipofanyikawaliongozawarshazakuwajengeauwezowatuwafamiliazilizoshirikiutafiti,na
Hatua Shughuli
Hatua 0
Familia zenye watoto wachanga zinaandikishwa katika makundi mawili tofauti lakini katika jamii zinazofanana
kabisa, jamii zilizo katika wilaya 5 tofauti; jamii kwa mtindo wa kubahatisha zinapewa jukumu la kuwa aidha‘Kundi
Linaloachiliwa’au‘Kundi Linalojengewa Uwezo’.Wazazi wanaambiwa kwamba ni utafiti unalenga kupata ujuzi wa
maendeleo ya mtoto; pasipo kuambiwa kiini cha utafiti wenyewe ili kuepuka uwezekano kuathiri matokeo ya utafiti
kwa namna yoyote ile.
Hatua 1
Wakusanya taarifa wanazitembelea familia zote zinazohusika katika utafiti mara 3, katika kila safari wakihesabu
maneno yanayozungumzwa kwa mtoto katika kipindi cha dakika 30 Utafiti wa KAP (Ujuzi, Mtazamo & Utendaji)
hukamilishwa katika safari ya 3 kwa kumwuliza mama wa mtoto mchanga maswali.
Hatua 2a
Familia zilizo katika kundi linalojengewa uwezo hupewa mafunzo ya kujengewa uwezo ya masaa 2 mara 3 wakiwa
katika makundi yanayofikia watu 30 (watu 3 kutoka katika kila familia hualikwa kuhudhuria mafunzo). Kundi
linaloachiliwa huachwa.
Hatua 3 Wakusanya taarifa huzirudia tena familia na kufanya tena hesabu za maneno mara 3, na utafiti wa pili wa KAP
Hatua 4
Wakusanya taarifa huzirudia tena familia zote watoto wanapofikia umri wa miezi 20-24 na kuwapima watoto kwa
kipimo rahisi uelewa wa lugha
Hatua 2b
Familia katika jamii za makundi yanayoachiliwa yanapewa mafunzo ya kujengewa uwezo kwa sababu za kimaadili,
lakini hii ni baada ya ukusanyaji taarifa wote kuwa umekamilika
Hatua 5 Taarifa zinafanyiwa mchanganuo, tamatishi zinafanyika, taarifa zinaandikwa na kutolewa
Jedwali1.
2 Page Folder Leaflet A4 Swahili version.indd 2 01/12/2015 08:29
3. Zungumza na Mtoto Mchanga
Matokeo
Unapochanganua taarifa zenye matokeo
yasiyolingana (yanayotofautiana), njia
bora ya kufuata ni kuchukua viwango vya
wastani au vya kati badala ya viwango
halisi vinavyoonekana. Thamani ya kati au
wastani inawakilisha kiwango cha chini
kilichopatikana kwa nusu ya vyanzo vya
taarifa, na hiyo itakuwa taarifa ambayo
haijaathiliwa na idadi ndogo ya vyanzo
vilivyoonyesha matokeo ya juu.
Jambo kubwa lililogunduliwa, kama
inavyoonyeshwa katika Jedwali 2 ilikuwa
kwambamazingirayalughayalikuwahafifu
sana katika vikundi vyote, ikiwa pamoja
na ukweli kwamba watoto wachanga
walizungumzishwamanenomachachesana
katika mwaka wao wa kwanza wa uhai.
Utafiti wa KAP ulibainisha kwamba wazazi
walikuwanauelewamdogosanakuhusiana
na umuhimu wa kumzungumzisha mtoto
tangu anapozaliwa, na namna hasa
inayofaa kwa kumzungumzisha mtoto.
Wazazi huongea zaidi na watoto kadiri
wanavyokua na kuwa na uwezo wa kuitikia,
kwa hiyo tungeweza kutarajia kuongezeka
katika idadi ya maneno yanayozungumzwa
kwa kila saa (mks) katika kundi lile ambalo
halikupewa mafunzo na miongozo ya lugha
kwa watoto wachanga katika kipindi cha
kwanza cha kuhesabu maneno (umri wa
miezi 9) na cha pili (umri miezi 19),pasi
na mafunzo yoyote. Kundi Lililoachiliwa
lilionyesha nyongeza ya maneno kutoka
mks 58 hadi mks 106, ambayo ni nyongeza
ya asilimia 83%. Kwa msingi wa nyongeza
hii ya asili, tungetegemea nyongeza katika
Vikundi vilivyowezeshwa ikue kutoka mks
65 ambayo ndiyo kiwango chao cha chini
hadi mks119. Hata hivyo, nyongeza kwa
kundi hili ilikua hadi kufikia kiwango cha
mks171.Hiiinawakilishanyongezayaziada
yaasilimia44%nyongezainayoakisifaidaya
mafunzo ya kujengewa uwezo yaliyotolewa
kwa familia husika.
Viwango hivi, hata hivyo, vimeonyesha
faida za warsha za kuzijengea familia
uwezo katika hali iliyo hafifu kwa sababu
matokeo ya viwango vya watoto ambao
wazazi wao walishindwa kuhudhuria
warsha za mafunzo ya kujengewa uwezo
yameathiri matokeo ya jumla. Kwa maneno
mengine ilishindikana kuzitenga familia
zilizoshindwa kuhudhuria warsha baada ya
kuwa zimeteuliwa.
Katika kupima ili kujua ni kiasi gani cha
lugha mtoto angeweza kukielewa, tuliweza
kuona kwamba katika maeneo ya Kundi
Lililoachiliwa kiwango cha wastani au cha
kati kilikuwa13/80, wakati kiwango cha
kati au wastani katika Kundi Lililojengewa
Uwezo kilikuwa bora zaidi kwa asilimia
77%, ambapo kiwango chao cha wastani
kilikuwa 23/80.
Mambo kadhaa ya faida yalipatikana
kutokana na utafiti wa KAP: kwa mfano,
ilikuwa bayana kwamba kile wazazi
walichojifunza kuhusu kuongea na watoto
kilitokana na maonyesho yaliyofanywa
na kisha wazazi nao wakafanya kwa
vitendo kile walichojifunza katika
maonyesho. Walijifunza kwa kutenda
kuliko walivyojifunza kwa kupewa habari
za kitaalamu. Licha ya taarifa, simulizi
kadhaa zilikusanywa na timu za utafiti.
Familia zilizo nyingi zilitaarifu kwamba
walipowazungumzisha watoto, watoto
wao walikuwa wenye furaha, na pia kina
baba walianza kuwa na ukaribu na watoto
wao wachanga walipoona jinsi watoto
wanavyokuwa na mwitikio chanya katika
suala la lugha.
“Ndiyo, tunaongea na watoto wetu
wachanga....lakini hasa pale wao wanapoanza
kutuongelesha”(mzazikijana,kablayakupewa
mafunzo)
“Ninaowatotowatano,lakinikwelininampenda
huyuhapa”(baba,baadayakujifunzakuongea
namwanaewamwisho)
“Nikiongea na mtoto wa miezi 6,
ninajiongeresha mwenyewe!” (mama, kabla ya
kupewamafunzo)
“Hatujawahi kuona mtoto mwenye akili
kama huyu” (mzee, baada ya ZUMM kufika
kijijinikwao)
kazi ya utafiti katika maeneo husika iliendeshwa na Asasi shiriki zisizo za Kiserikali zinazoshughulikia maendeleo ya awali ya mtoto. Mradi
kwa jumla uliendeshwa na shirika la Children in Crossfire, asasi isiyo ya Kiserikali iliyosajiliwa nchini Uingereza yenye makao yakeJijini Dar
es salaam. Janet na David Townend ambao ndio Waanzilshi wa shirika la ZUMM, waliandaa mfumo wa utafiti, walitayarisha nyaraka na
vitendea kazi vilivyotumika katika utafiti, walifanya kazi kwa ukaribu wakishirikiana na mtafsiri wa nyaraka, waliwatembelea wadau mara
kadhaa ili kutoa mafunzo kwa timu za wakusanya taarifa na wawezeshaji wa utafiti.
2 Page Folder Leaflet A4 Swahili version.indd 3 01/12/2015 08:29
4. Tamatishi na hatua zitakazofuata
Shukrani
Idadiyamanenoyaliyozungumzwakwawatotoyaliongezekakadiri
siku zilivyoongezeka katika makundi yote mawili, kama ambavyo
ingeweza kutarajiwa kwamba watoto wanavyokua ndivyo
wanavyokuwa na mwitikio mzuri. Lakini wale waliohudhuria
mafunzo walionyesha kuwa na ongezeko kubwa zaidi la maneno
kuliko watoto katika Kundi Lililoachiliwa. Uelewa wa lugha wa
watotoambaowazaziwao walipewamafunzo ulikuwa naviwango
vya ubora zaidi kuliko watoto katika Kundi Lililoachiliwa.
Wazazi nchini Tanzania hutumia maneno machache zaidi kuliko
katikanchinyingineyoyoteambakohesabuyamanenoimefanyika.
Kiwango cha chini cha mks 63 kinachozungumzwa kwa watoto
wachanga ni cha chini mno ukilinganisha na viwango vya maneno
kwa saa vinavyopatikana katika tafiti kama hii katika nchi
zilizoendelea: mks 600-800 katika familia maskini na hadi kufikia
kiwango cha hadi mks 2,000 katika familia za wale wenye ukwasi.
(Kwa kulinganisha, watu huzungumza takriban maneno 120 kwa
dakika)
Matokeo haya yanaonyesha kwamba upo umuhimu kwa ujumbe
wa ZUMM kuifikia jamii hasa tunapozingatia umuhimu wa ujuzi
wa lugha wa awali katika matokeo ya ujuzi wa kusoma na wa
kielimu katika siku za baadaye za mtoto. Habari njema ni kwamba
kikwazo kikubwa kinachowazuia wazazi wasiongee na watoto wao
wachanga ni hali ya kutojua namna ya kuongea na watoto wao
wachanga, na pia kutojua kama upo umuhimu wa kufanya hivyo.
Mara wazazi wanapoambiwa ukweli wa jambo hili na kuonyeshwa
namna ya kuzungumza na watoto wao wachanga, wengi wao
hubadili tabia au mwenendo wao. Kwa kuwa mtoto naye humlipa
mzazikwakuitikiakwatabasamunasautizafuraha,tabiahiimpya
huendelea na kukua na mara nyingi kuenea hadi katika familia
nyingine za jamii husika.
Sasa tunao ushahidi wa kutosha kutuwezesha kuzitendea kazi
jumbe za ZUMM kupitia mfululizo wa jitihada zitakazoilenga jamii
chini ya mwavuli utakaojulikana kama ‘ZUMM kwaVitendo’. ZUMM
na CiC ni wadau washirika katika sehemu za utangulizi za mradi
huu, mradi utakaotoa mafunzo ya kuwajengea uwezo kwa njia
ya mtandao na pia kuwapa vitendea kazi wataalamu walio katika
taaluma hii ili waweze kuchukua jumbe za msingi za ZUMM na
kuzieneza kwa jamii NchiniTanzania.
Kinachohitajika sasa ni kuufikisha ujumbe wa ‘Zungumza sana
na mwanao mchanga katika njia sahihi tangu anapozaliwa’, kwa
wazazi na familia kote nchini. Haikughalimu kitu kwa wewe
kuongea na mtoto wako mchanga; ni jambo ambalo hata wazazi
walio maskini sana waweza kulifanya ili kuongeza uwezekano wa
majaliwa mema ya watoto wao maishani.
ZZUMM na CiC wanashukuru kwa msaada wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, na
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa juhudi zilizofanywa na wizara hizo katika kuruhusu na kuupa utafiti huu jukumu teule.Wanapenda
pia kuwapa washirika wao wote wa hapa Nchini shukrani nyingi kwa kazi yao ngumu, pia bila kusahau tunachukua fursa hii kuwashukuru
kipekee UBS Optimus kwa msaada wao wa kifedha uliowezesha kufanikisha utafiti huu.
Kwa habari zaidi kuhusu ZUMM nenda katika tovuti: www.childrenincrossfire.org/programmes/talktoyourbaby
or email jantownend@gmail.com
Kwa habari zaidi kuhusu CiC nenda katika tovuti: www.childrenincrossfire.org
Maneno yazungumzwayo
kwa mtoto kwa saa
Kipimo cha Uelewa
wa Lugha
Angalizo:
CG = Kundi achiliwa
IG = Jengewa Uwezo
Kiwangocha
chini
Maendeleo
%Ongezeko
toka
kiwangocha
Chinihadi
Maendeleo
Alama/80
Uwiano
IG/CG
Watoto
wote
wastani 63 133 111 18
Watoto
wote
CG/IG
Ulinganifu
CG wastani 58 106 83 13
1.8
IG wastani 65 171 163 23
Jedwali2.
2 Page Folder Leaflet A4 Swahili version.indd 4 01/12/2015 08:29